Friday, July 06, 2007

Diaspora return! - Housing Situation

Waungana,
First thing first: Mtu ukishatua... cha kufanya ni kutafuta pa-kujibanza! Soooo nianze na makazi...
Labda niseme tu... situation yangu ilikuwa tofauti kidogo. As a "displaced" person sikuwa nimejitayarisha na ka "jengo" hapa nyumbani. Baada ya kufanikisha maswala ya "ganda" huko US, niligawa visehemu nilivyokuwa navyo kwa brothers & sisters... - unajua tena. Wakati huo mambo yalikuwa "Mimi Bongo ndo basi tena!" And so hata viwanja nilivyokuwa nimetafuta, niligawa kwa mabwana wadogo etc...
With the benefit of a hind site (wenyewe wanasema hindsite is always 20/20)... nataka tu kukubali kuwa... huo kwa kweli haukuwa msimamo wenye faida kwangu. Unajua kuna ujana na ujana... na kila ujana una mambo yake. Kuna baadhi ya vijana wapo very smart in this area... mimi sikuwa mmojawapo... Hata hivyo, bado kuna chance.. I mean, tunajifuna kutokana na makosa - na maadamu bado tunaishi... "one day yes!"
IN 2006 nilikuja kujaribu kuangalia uwezekano wa kujiweka sawa kabla ya kuja kwa kutafuta japo eneo la kuja kujenga baadaye. Tatizo... machale yakanicheza, nika- chicken out, nikidhani wajanja walikuwa wengi na bei za ka"ki-ploti"zilikuwa "si zenyewe".

Well... freebie of the day!!! Ardhi (na hasa hapa Dar) ni deal ile mbaya!!!! na kwamaoni yangu kwako msomaji, kama huna ka-ploti... fanya juu chini ukipate sasa my friend! Kama una-ka-ploti, lakini hujajenga... jaribu kukamilisha sasa- it is as simple as that!

IN anyway... Kufika hapa ikabidi tuanze kutafuta nyumba ya kupanga! Ni kitu kinachojulikana hapa kuwa ili upate nyumba ni lazima utumie "madalali" (agents)

kwa jinsi tulivyopanga, tulikuwa tunataka kupata maeneo ya Mikocheni, sinza, Kijitonyama, Makumbusho, Msasani etc. Tulidhani ni maeneo mazuri (karibu na mjini:) TATIZO... maeneo hayo ni ghali sana. Kwa mtu unayetaka nyumba ya vyumba 3 (of course with a sebule & a small place to pack your "makopo") you should be looking to shed the upward of $1000 a month (payable in advance on an annual basis) na hiyo unaambiwa ni bei ya "mzawa"! second tatizo...katika maeneo hayo you will be quoted prices in US$
Perhaps what has been the most difficult thing is to try and convince a dalali (and a homeowner) the fact that, not all ya wanao "toka mtoni" wanarudi "loaded"///na kwamba atu kama sisi... ni kweli kuwa hatuna $$ nyingi za kutumia. Tatizo ni kuaminika kuwa kweli huna kitu... I mean... wewe umetoka majuu (kwa Bushi)...what do you mean you do not have money?
IN anyway... ngoja niishie hapa....

talk to me!!!

Wednesday, July 04, 2007

Hodi Hodi Bongo!!!

Waungwana,
Hodi hodi kijiweni...
Awali nianze kwa kuomba radhi... It has been a VERY long time tangu ni post anything here (sina hata uhakika kama bado kuna mtu hapa kijiweni).
Well... Unajua tena maisha... Nilifanya uamuzi kurudi Bongo (baada ya takribani miaka kibao huko ughaibuni)...Sikufukuzwa ,na wala maisha haya kunishinda huko (niweke wazi kabisaaa.... maana waswahili wataanza vineno) kama huamini uliza uliza! In "eneway" nilijikuta nimekabwa koo vibaya sana katika kujitayarisha... I mean... mtu umeajiriwa, un akazi za watu na hivyo unajitahidi usije ukaharibu mwishon... at the same time unajaribu kujiweka sawa usije ukaangukia "mwanguko wa mende"... tough nut!!!

In "eneway" nipo Bongo!!! Na kama nilivyoweka kwenye blog "dada" Tanzanian Development Connection nimewasili hapa takribani mwezi sasa... najua wenyeji mtauliza... vipi mbona kimya (?) Sasa wazee simnajua kuku mgeni... hata barazani kwenyewe nilikuwa sipajui.... kidogo kidogo, tunaanza kutokeza pua nje kidogo - at least kuliona jua, nakunawa uso (matongo-tongo kibao)
Kuacha hivyo...Bongo kupo... Wiki chache baadaya kutinga hapa, jamaa mmoja alitahadharisha "Ukija hapa inabidi uingie ki-bongo bongo, ikija ki "unene unene" jamaa ni lazima wakulambe kidogo" Yaani kama jamaa alikuwa anatabiri vile... 2 days later, jamaa waliniingiza mjini na ka-razr kangu nilichokuja nako toka "majuu" kakatoweka "katika mazingira ya kutatanisha"!
Kilio both sides: 1. bei ya ka-razr kwa kweli ina "gandamizaga"... kuipata nyingine kazi (na hapo uwe tayari kuuziwa "sample" au a "knock off" 2. Ni zile information nilizokwisha kuzi save...
Yaani nilijikuta najisemea mwenyewe:
Razr - with memory card $300; SIM card - $1
Information ndani ya simu... 'Priceless"

Ndo Bongo hiyo!!!! Yes, kuna mengi ya kujifunza... Lakini it is Home!!! Na kama wanavyosema "East or west, Home is best! IN addition... I think I can see a tiny tiny tiny light at the other end of this tunnel!!!

Hey, any blogger in Dar? ... tufanye tukutane live basi; wageni tunakuja na shida zetu, lakini msitukimbie jamani:)) Michuzi upo mzee?? Nasikia na Jeff yupo hapa

talk to me...
Ned
Peace
ned