Wednesday, May 17, 2006

Emile Augustine Muta AFICHULIWA!!!

Hii story nimeinywa nzima nzima toka wabongo Yahoo group- group ya wabongo hapa Columbus Ohio.

..., tulikuwa tunajiuliza huyu jamma ni nani? Soma story chini hapo!

Habari za mapumziko ya mwishoni mwa wiki watanzania wenzangu na hasa wazalendo.
Narejea tena hewani kama nilivyo ahidi hapo awali kuhusu anayejiita mkimbizi toka Tanzania bwana Emile Augustine Muta.
Narejea tena kusema The Kilimanjaro empire imekuwa na mipango ya muda mrefu sana hasa ukizingatia kabila la Watutsi walivyotapakaa Afrika mashariki na ya Kati kama sio Afrika yote.
Ndugu huyu kama wengine walivyokuwa wanajifanya Watanzania kumbe wamekuja katika shamba la bibi, yeye na wazazi wake wote walikuwa katika kambi ya watutsi iliyokuwa huko Nkwenda Wilaya ya Karagwe Mkoa wa Kagera.
Kama mnakumbuka wakati huo wa Mwalimu watu hawa walipewa huduma sawa na watanzania wengine kuanzia elimu hadi matibabu, na hivo ndugu huyu alisoma Tanzania, na kisha alipata kazi serikalini kama wengine wengi tulivyo waona.
alifanya kazi jijini Dar kwa muda mrefu, lakini baadae alihamishiwa Mkoani Tanga ambako yeye kutokana na kukosa uzalendo na kujali maslahi binafsi, aliugomea uhamisho huo na kuamua kutimkia huko Marekani, ambako kuna dada yake na kisingizio cha kwenda kusoma.
Hajawahi kukamatwa na kutiwa ndani hata mara moja, kwa kuwa serikalini ukiondoka bila ruhusa basi kazi imekwisha na ndicho kilichofanyika kwa ndugu huyu.
Akiwa huko Marekani mwanaye alifariki dunia, yeye hakufika katika msiba huo hadi pale mkewe naye alipofariki dunia ndipo jamaa alikuja kwa muda mfupi kuhudhuria japo, alikuta wamekwisha zika.
Baada ya mazishi jamaa alirejea Marekani, ni kweli kwa mtu anaetafutwa hilo lawezekana na asikamatwe?
Hiyo ndiyo historia fupi ya mtu huyu ambae anatafuta maisha kwa kusema uongo na kulipaka matope taifa letu kwa maslahi yake binafsi. Mtu huyu na wengi kama yeye hawana uchungu na nchi yetu, na ndio maana yuko tayari kufanya chochote bila kujali maslahi ya Tanzania na watanzania kwa ujumla. Anadhani hakuna mtu au watu ambao wangepata kuona habari hizi wakati sasa hivi Dunia iko katika ncha za vidole na hakuna siri.
wanapo sema anaelimu nzuri ni ipi hiyo? mimi ninajua wakati anatimkia huko alikuwa na diploma ya sheria ya Mzumbe!
Ni kweli alikuwa anaheshimika na kabila lake kwa kuwa alikuwa anajitahidi kulinda maslahi yao.
Inatia uchungu sana kuona fadhila zetu sasa zimekuwa ni kupigwa mateke. Imefika wakati sasa sisi watanzania wachache wenye upeo wa kuona mbali kukemea hili, na hata kuwaumbua watu kama hawa kwa kuwasiliana na taasisi walizozidanganya ili kusafisha jina la nchi yetu katika medani za kimataifa.
Kwa leo naomba niishie hapo, naomba niwasilishe.
Ziota.

Thursday, May 11, 2006

Wabongo wengine bwana!!!!! - Inabidi tubadilike

Waungwana,

Awali kabisa ni lazima niweke wazi kuwa sina uhakika kama huyu Emil ni mBongo! Sio tu inakuwa ngumu sana kwangu kukubali kuwa waTz tumefikia kiwango cha chini namna hii; bali pia kutokana na ukweli kuwa Emil hakutumia jina lake la mwisho... na hivyo inakuwa ngumu sana kuhakikisha kama yeye ni mTz; au ni mtu wa kuja anajaribu kutumia mgongo wa wengine... Uwezekano huu wa jamaa kutokauwa mBongo ndio unachochea nia yangu ya kuandika kama ninavyoandika hapa (ambapo nitaandika kwa kuassume kuwa jamaa ni mmbongo - kama alivyodai).

Nina amini kabisa kuwa sote (waTz) tuna wajibu wa kumuumbua mtu yeyote anayejaribu kujinufaisha kibinafsi kwa stories za kipuuzi zinazogharimu heshima yetu waTz kama watu waaminifu (ukilinganisha na mataifa mengine tunayoyajua - naogopa kushtakiwa:). Ninachosema ni kuwa kama jamii ni lazima tuwe tayari kuumbua tabia kama hizi! Hata kama mimi mwenyewe ningefanya kama huyu bwana au nitajikuta nimefanya kama huyu ndugu yetu - nitastahili kufanyiwa hivyo hivyo!

Sasa nafahamu kabisa umuhimu wa kuonyesha huruma, na upendo n.k n.k. Nafahamu wengi tuliopo huku ughaibuni... wakati mwingine inabidi mtu uwe "underground" n.k n.k. Lakini ni vizuri kukumbuka kuwa jamii ni jinsi tunavyoitengeneza wenyewe! Ukimya kwa kitu kama hiki sio jibu.

KWa maoni yangu...huyu bwana tapeli period!
Kwake yeye faida yake Binafsi, haina bei! Hata kama ni kuwaibisha waTz milioni 38; kwake yeye heshima na credibility yetu sote kama taifa - kwake yeye ni gharama ndogo sana ukilinganisha na tamaa aliyonayo - Kiurahisi kabisa... inaonyesha jinsi "ubinafsi" ulivyojikita ndani yake! ... What a looser!
Sasa tufanye nini?
La kufanya ni kumtoa hadharani! - Yes, najua baadhi mtaniona "noma" au "kinaa" au ...whatever man! I am just disgusted by his behavior!
Ndesanjo amelalamika kuwa hicho kitu hata hajakisikia... ndugu, ndio utapeli wenyewe huo...hiyo story nifix babu kubwa! Dawa = nikumuibua peupeeee!

Iwapo kila mmoja wetu atatuma email kwa mwandishi (ambaye nadhani ni mchungaji wake) na kwa mhariri wa gazeti la The Lutheran - nadhani watapata ujumbe!
Kuhusu mhariri, tutie shinikizo la kumwomba atumie njia zozote anazozifahamu - ikiwa ni pamoja na kuwasiliana na KKKT (ELCT - Eveng. Lutheran Church of Tanzania); kupata uhakika wa story ya Emil.
Halafu, sidhani kama itakuwa too much kumtaka aweke story nyingine ya kuwafahamisha wasomaji wake kuwa the whole story of Emil was a shameless, lowly and cheap scam against the people of Tanzania.
Huenda I am taking this too personal! Lakini kama mtanzania - hasa ninayeishi huku ughaibuni... najisikia kama vile mtu kanitukania mzazi wangu!

Kibaya zaidi ni kuwa... kwa story kama hii, hata kama kuna watu walikuwa wana nia ya kweli kabisa kusaidia waTz waliopo huklu ughaibuni - au hata nchi kwa ujumla...sasa inakuwa ngumu kwa sababu ya upuuzi wa mtu mmoja!
In anyway jazba pembeni:
Aliyeandika hiyo article ni Mchg. Charles N. Bailey wa kanisa la Kilutheri "All Saints" Lutheran Church Auburn Kent, Washington; ambaye nina hakika ni mtu mzuri anayejaribu kusaidia waumini wake kwa kila namna anayoweza. Ni kwa vile tu tapeli amempata!
Inawezekana kabisa wewe na mimi ndio tegemeo pekee la hawa wazungu wa watu kuupata ukweli wa mambo! Aidha kwa Mchg. Bailey - hili linaweza kuwa bomu kwake! Hebu fikiria iwapo msharika mmoja atapata taarifa kuwa jamaa tapeli... unadhani itakuwa shida kufikiria kuwa huenda Emil ana njama na Mchg? In anyway, kuwaandikia si kuwatia aibu ni kuweka wazi na kupasua jipu ambalo tusipo fanay hivyo matokeo yanaweza kuwa mabaya zaidi!
Sikuweza kupata email binafsi ya Mchg. Lakini contacts za hilo kanisani ni:
27225 Military Rd S
Auburn, WA 98001-1808
Simu: 253-852-4884
email: aslcauburn@comcast.net
Mtandao: http://www.aslcauburn.com/index.htm

Kuhusu The Lutheran magazine. Email ya mharirini: utheran@thelutheran.org

Ned

Unakaribishwa kijiweni II

Waungwana,
Ili kutimiza nia ya kuruhusu watu kuweza kutundika "stories" hapa "Kijiweni", Inabidi nikualike rasmi.
Tafadhali jisikie huru kuweka comment yenye anwani yako ya email ili nikutumie ukaribisho.
Ndesanjo & Mwaipopo, nashukuru sana kwa kunitembelea.. karibuni sana wazee
Ned

Wednesday, May 10, 2006

Baadhi yetu Wabongo inabidi tubadilike!

Rafiki yangu mmoja amenitumia hiki kisa cha huyu jamaa "Emil" anayedai kuwa mTz. Kwa ufupi jamaa ni fix tupu! Au sijui niseme ni noma kichizi! Stiry yake ni ya uongo usio na kifani. Ati amekimbia Tz kwa sababu ya fujo za kisiasa - eti kwa sababu alikuwa ameamua kutenda haki kama mkristo safi.
Jamaa kaja Marekani - kawazuga wazungu (kulia, kushoto, kwetu kinyerezi, baba kwame ni mjomba wangu) wazungu wamelewa hata haisimuliki!

Story imeandikwa kwenye gazeti la kilutherani "The Lutheran"

Story inaanza:
"...Meet Emil. Like Job of the Old Testament, he has been tested and blessed by a God of grace and unconditional love.
That our paths should meet at all reflects God’s creative genius—and a divine sense of humor. Imagine a God who weaves together the stories and hearts of a small Lutheran church (of Scandinavian descent) in the Seattle area and the story and heart of Emil, a stranger from Tanzania. Tragedy and redemption, loss and blessing, faith and restoration. That’s Emil’s story—and now it’s ours too.
....Emil Augustine was a well-
educated 36-year-old who held a prestigious position in the Tanzanian government. He had a nice home, two growing boys and a wife who worked as a nurse. He was respected in his tribe and traveled the country using his ability to speak five languages.
Then his life began to unravel.When a new political party took control, he was instructed not to give visas to any of the opposition’s leaders. A Christian, Emil chose to uphold the Tanzanian constitution, which allowed any citizen of good standing to leave the country. After one warning, he was arrested and thrown in jail without trial..."
Waungwana, jisomeeni mwenyewe hapa. Uongo bin nuksi!
Ni nini maoni yako? Kama mtanzania, nini tunaweza kufanya kujikinga na watu kama hawa? By the way huyu jamaa ni mtanzania kweli?
Mawazo yangu ya nini wee na mimi tunaweza kufanya kukomesha hii nuksi = next posting.
Ned

Karibu Kijiweni

Karibu sana "Kijiweni"

Nilipokuwa Bongo - ilikuwa si ajabu kunikuta mitaani, tume "ganda" na washikaji! tunashirikiana michapo (stories). Tulikuwa tukikutana "kijiweni".
Ukifika kijiweni, ni stories baada ya story. Nyingine ni ndoto za maisha, mikasa inayotokea mitaani, nyingine za kufurahisha nyingine za kusikitisha... mradi kila kitu kimo. Hakuna ajenda...mtu unatoka nyumbani huna uhakika utakuta story gani huko kijiweni; lakini ilikuwa ku-miss ni pigo kubwa. Wengine wanaweza kuita sehemu kama hii "Ukumbi wa makoroma" au "barazani"... La muhimu...: Unakaribishwa sana kushiriki!

Kama kawaida "A few ground rules" (Masharti machache ya matumizi):

Masharti YOTE ninaweza kuyaweka katika neno moja:HESHIMA

1. Heshima ni kitu cha bure. Tafadhali andika kama unazungumza na mtu aliyesimama mbele yako - na mnajuana kikamilifu.

2.TAFADHALI jaribu kujiweka wazi... kwa kweli hakuna haja kabisa ya kujificha ficha nyuma ya majina kama "Anonymous" - By the way, unajua kuna namna ya kutambua jina la mwandishi (hata kama emejificha kwa kutumia an alias name)? Kutumia "Anonymous" haimaanishi mtu akitaka kukujua hawezi!

3.Maswala yote yanayohusu unyumba, uchi na vitu kama hivyo hayatavumiliwa hapa "kijiweni" Kama unasoma maandishi haya una umri wa kutosha na bila shaka unaelewa kabisa ninachokisema!

4.Kwetu waTz - tunaheshimu "kichwa chenye mvi". Baadhi yetu huwa tunapata "Mshtuko wa moyo" tunapoona watu wanadharau wazee wanaojulikana ni wakubwa kiumri. Kweli tunatumia "keybodi" kuwasiliana... lakini kuna watu wanafahamika kuwa wenye mvi (mfano viongozi wa zamani ambao wamstaafu n.k. Tafadhali tumia busara na kuonyesha heshima.

5.Ni marufuku, kutukana, kuapa, au kuweka maandishi au picha inayojaribu kuonyesha kadamnasi kwamba wewe ndio umekasirika kichizi!

6.Changia au shambulia wazo... sio utu wa mtu!

Masharti haya nafuu ni kwa faida yetu wote.... Uvunjaji wa masharti haya nafuu hautavumiliwa! Na kama mwenyeji wako itabidi tukufungie nje!

Mwenyeji wako
Edmond